Saturday, September 15, 2007

GLOBAL PUBLISHERS MMMMH !!!?? HADITHI HII KAWAFUNDISHA NANI?

Si Kawaida yangu kuanza kaundika jambo linalonikera ghafla lakini hili nimeshindwa kuvumilia. Nilipata kukutana malumbano kati ya Chahali na watu wa Globalpublishers wa Tanzania.
Katika malumbano yao niliona bwana Chahali akiwa na hoja nyingi zenye msingi katika hilo swala waliliokuwa wakibishania(kwa upande wangu). Ingawaje nilikuwa msomaji tu lakini maoni yao wote yalikaa kichwani mwangu.
Kilichotokea sasa ni ijumaa moja ya gazeti linalochapishwa na globalpublishers lilitoa picha ambayo ilileta utata (hasa kwangu mimi) na wengine kuhusu uwezo wa watoa habari hawa kwani hizo picha nilipata kuziona kitambo sehemu nyingine. Kilichonishtusha ni kuwa zilitumiwa kama ni habari mpya iliyotokea huko nyumbani. Baada ya kusoma hizo habari nilisema kweli sasa tumekwisha...yaani hawa wachapishaji wanafanya kitu kama hiki? Nikamkumbuka Chahali ni kasema hapa hana tena la kujitetea ni kuacha mwenye macho atazame. (Chahali nakuunga mkono aslimia 200! kwa magazeti ya Udaku). Kweli kwenye uongo ukweli ujitenga.
Nashukukuru kwa watu wengi kuwatolea macho hadi wao wamefuatilia hilo swala na kulifanyia kazi soma hapa na hapa.
Inatia aibu sana na ndio maana nilaandika kuwa ni vizuri mara nyingi kujiuliza Hadithi hiyo kakufundisha nani?

Thursday, September 13, 2007

WADUDU NA MADEREVA NA JAMII

Inasemekana sisimizi au siafu au nyuki hana uelevu sana kama inavyofikirika kuwa nao. Ila kundi la sisimizi/siafu/nyuki ndio linauelevu (umenipata hapo?)... Yaani hilo kundi linaweza kutatuta tatizo ambalo kama huyo sisimizi/siafu/nyuki angekuwa peke yake isingewezekana. Kama kutafuta njia fupi ya kwenda kutafuta chakula, kuwapanga wafanyakazi kwa kazi ,mbalimbali au kuwa walinzi wa sehemu waishiyo. Yaani wakiwa mmoja mmoja wanakuwa madunya ila wakiwa pamoja wanachangamkia tatizo haraka na kwa makini kwenye mazingira yao. Kufanya hadithi fupi ni kuwa watafiti wa wadudu hawa wamegundua kuwa hakuna ambayo ndio Kiongozi ila maamuzi yanategemea na jinsi wanavyo wasiliana. Soma hiyo habari hapa.
Utajiuliza sasa ikiwa hivyo ndio nini? Mimi napenda kuhusisha tabia hiyo na ule utaratibu wa madereva (Wa Tanzania) kuwashiana taa, yaani wanapeana ishara pale magari yanapopishana ndio wanawasiliana kuwa nanukuuu maandishi ya Ndesanjo kuwa,"katika zile alama za madereva kuna alama za kuashiria kuna "mkusanya kodi" mbele (yaani askari wa "usalama" wa barabarani (au usalama wa mfukoni). Halafu kuna ishara ya kuwa kuna "vichwa" (yaani abiria huko alikotoka". Yasome hapa. Sasa sijapata kuja lipi ndio huwa ni zaidi. Kwa mtazamo wangu madereva waliweza kujigundulia utaratibu mzuri sana wakupashana habari ya nini cha kufanya baada ya kuwashiana taa. Wao wako kama hawa wadudu na ukiwa peke yako huna ujanja ila mkiwa wengi mnaweza kupashana habari kuepushana na unaloliona wewe kuwa ni Shari.
Lengo la hadithi hii ni kukandamizia kuwa kuna njia nyingi za kusaidiana ili kuondoa tatizo kama wanfanyavyo wadudu au madereva (ila siwaungi mkono kwenye swala la kupindisha sheria za barabara)...Umenipata hapo?

Thursday, September 06, 2007

Prof.CHACHAGE, MAMA TERESA

Kama wewe huwa unapita pita hapa kibarazani kwangu utakuwa unashangaa aaah! huyu Ndabuli naye kwa kutofuata ahadi zake ni kiboko ( kivipi?). Si kwenye mtundiko uliopita alisema atazungumzia zaidi kuhusu kisa cha kununua kahawa kwenye bar na Kuhusu kuwashiana taa kwa madereva ..huyu bwana ....#¤%& ....kabisa na hata kwa waliotoa maoni alisistiza hivyo...( kama wewe ndio umenitembelea leo soma makala hiyo ya chini) au bonya hapa.
Ni kweli nimetoa hiyo ahadi na nitaitimiza, ila jambo lingine limenikuna sana nikaona ngonja niliandike hili kwanza...(najua unajiuliza jambo gani tena!)
Wiki hii nimemkumbuka professa Chachage. Nikiwa huku ugenini nilipata kukutana na prof. Chachage akiwa katika mizunguko yake ya kutoa mihadhara mbalimbali. Basi nami nilikuwa mmoja kati ya watu waliohudhuria shughuli ile iliyomleta... siku moja (kati ya siku zile alizokuwa hapa) nilipata/tulipata wasaa wa kukaa naye jioni huku tukipata moja moto moja baridi ..(mmh nimesahau moja baridi nyingine baridi maana huku hakuna za moto..labda chai na kahawa). Katika mazungumzo yetu ya jioni kuhusu mambo mbalimbali ilifika wakati tukiwa tukijadiliana (kulikuwa na wadanganyika wenzangu...oops watanzania wenzangu) likatokea swala moja la kupingana na magazeti yanayoashabikia siasa nizisozipendelea sana.
Huwa na kawaida ya kusubscribe (sijui kiswahili chake jamani..si uniambie kama unajua) magazeti na majarida mbalimbali. Kati ya hayo kulikwa na jarida, sijui gazeti, la Time ambalo hutoka mara moja kila wiki. Baada ya kulisoma kwa muda mrefu niliamua kuachana nalo kwani niliona vingi vinavyoandika humo haviendani na mtazamo wangu, hivyo nikaamua kutolilipia tena...basi prof. Chachage aliposikia hivi aliniambia kitu kimoja sitosahau mpaka leo. Kuwa ni makosa makubwa sana kutosoma mtazamo wa mtu mwenye itikadi ambazo hukubaliani nazo..unakuwa katika mstari mzuri wa kumjua au kujua fikira zake na kuweza kuzipambanisha na zako kwa kumsoma mtazamo wake... nami kweli nilikubaliana naye hiyo niliendelea kusoma lile gazeti la Time(ila niliacha kulilipia.. siku hizi nalisomea makataba).
Gazeti la wiki hii (lenye tarehe ya septemba 3) limekuja na kitu ambacho kinalingana na kitu nilichoandika zama zilizopita kikiwa na kichwa cha habari Imani zetu inakuwaje? Makala yenyewe inaelezea kuhusu Mama Teresa (Unamkumbuka? yule sista wa kikatoliki...enhee yule mshindi wa nishani ya Amani ya Nobel ya mwaka 1979) Msome hapa. Kwamba kwa takribani miaka 50 hakuona uwepo wa mungu.
Katika kitabu kilichotolewa chenye Jina la Mother Teresa: Come Be My light. ambacho kwa wingi kina maelezo ya mawasiliano kati yake na wakubwa zake. Kinaonyesha kuwa kwa karibu nusu muongo wa maisha yake hakuona uwepo wa mungu kwa hali yoyote. Hii ni makala iliyonifikirisha sana. Basi nisimalize uhondo soma mwenyewe makala hiyo hapa. halafu jifikirishe..Baadae!

Monday, July 30, 2007

CHAI,ZAMBARAU NA FULLLIGHT !

Anti: Karibuni, Karibuni,Karibuni ngoja niwaongezee kiti
Ndabuli: Asante Anti, du anti umependeza!
Washikaji wa Ndabuli: Wanacheka..
Anti: We anko(anamjua jina lake) unacheka nini sasa?
Mshikaji 1 wa Ndabuli: Yaani we Hadija leo unaniita anko?
Mshikaji 2 wa Ndabuli: Hube tulete vinywaji hizo longolongo zenu mtaongea wakati tunakata kiu.
Anti: Anko unakuywa nini?
Ndabuli: Naombaaa (nasitasita)....
Mshikaji 2: Kunywa Kilimanjaro au Tusker
Mshikaji 1: Kunywa Serengeti ndio yenyewe...mletee Serengeti darling wangu!
Anti: (Huku anacheka) Koma wee mie Darl wako leo, (anagongea mkono pwaa na mshikaji 2 )sitaki kabisa utani wako, haya sema na wewe unakunywa nini?

Mshikaji 1: (tena kwa msisitizo na sauti kubwa)Kahawa !
Anti: Kha, unanini leo wewe, mkeo leo kakufumania nini au umerukwa na akili wewe.
Ndabuli: Kwani hamuuzi kahawa hapa?
Woote jirani yetu: Wanacheka !haha haha! haha!

Basi nisiendelee sana ngoja niseme...mmhh hapana niandike, hadithi inataka niseme nini? Huku ugenini kwenye sehemu ya kinywaji unaweza pata Kahawa, chai. Sasa katika safari yangu ya nyumbani katika maongezi na ndugu jamaa na marafiki tulifika wakati tukaongelea hili jambo basi tukasema hebu tukiwa siku moja tunakwenda kupooza koo tujaribishe halafu tuone itakuwaje..basi ndio ikawa hiyo watu walibanwa mbavu kwa kucheka-
Basi mjadala ukaanza.... kwanini wasiuze kahawa na chai hapa-nakwambia kila upande ulielekea kushinda...
Ila swala langu ni moja tuliweza kuanzisha mjadala ambao wengi wetu tulichangia na kuendelea kupooza koo kwa furaha kabisa (na mpaka mwenye sebule ile tukamwambia ajaribu kuaanza hii biashara tuone itakuwaje?)..Ntaendelea na hiki Kisa baadae

Umeisha safiri na kwa kutumia Barabara kutoka mkoa mmoja hadi mwingine? Si unakumbuka kuona madereva wanawashiana taa au kupungiana mikono huku wakionyesha alama fulani? ..na wanaelewana hebu jiulize au waulize kama walifundishwa maana zake wakati wa mafunzo ya udereva... aaa wapi? Lakini mbona wanaelewana... na hili nitalimalizia baadae

EGIDIO Kaniuliza mambo 8 msiyoyajua juu yangu.

1. Sijui vitu vyote msivyojua kuhusu mimi.
2. Naogopa sana mkijua vitu msivyojua kuhusu mimi.
3. Naogopa sana kupigwa picha.
4. Akina Dada wote naokuwa na urafiki(wa kimw....) na mimi (akina Stella)baada ya muda(au tukimalizana) wanaolewa. ...mhh mwajameni!
5. Akina stella wangu wote tuliokuwa pamoja tulianza ghafla urafiki.
6. Napenda sana Kula chips dume(mihogo ya Kukaanga).
7. Nilisimamishwa shule kwa mara ya Kwanza nikiwa darasa la nne.(Kwa sababu ya kugoma kuchapwa viboko nikiwa nimevua kaptura mbele ya wasichana- nilikamatwa nimepanda mti nikidondosha zambarau!) ...mmh mwanawane!
8. Rejea namba mbili.

Alamsiki


Wednesday, July 18, 2007

Wednesday, June 13, 2007

NIKO NYUMBANI (yaani niko Tanzania)

Jamani, kimya hiki kisiwatishe sana kwa sasa niko Tanzania, nakata mikoa na ndio maana sionekani huku.
Ni kitambo nilikuwa sijatemebelea nyumbani basi muda mwingi unatumika katika kusalimia ndugu, jamaa na marafiki pamoja na kudodosa mambo kadha wa kadha ambayo nayaona.
Tatizo moja ni kuwa muda mwingi ndio huo natumua kucatchup na jamaa na kuonja zile larger!!! .. muda wa kukaa na kuandika kidogo haupo na vilevile si niko likizo jamani...(au kublog hakuna likizo?)..mmmh na mitandao huku mingi iko taratibu (basi muda wa kwenda kwenye kikao unapungua) sana sana nasomea kwenye simu yangu ila kuandika ndio ...hapa.. basi natarajia nikitulia nitaendelea kutoa nikifikiriacho..
Karibu tena

Monday, April 23, 2007

Nimerudi tena Jamani. Baada ya kufuta vumbi nyumbani na kusalimia mtaani nikaona ngoja niwabeep (au niwa dipu kama anavyosema Chesi Mpilipili) wale walionitembelea wakati sipo na kuacha ujumbe na wale waliopita kimyakimya. Katika mihangaiko yangu nilifika pale Parisi, Ufaransa na nilitembelea ule mnara wao maharufu (ingawa walitaka kuuondoa mwanzoni) wa Eiffel. Kilichonifurahisha pale Kileleni niliona wameonyesha ni umbali gani uliopo kutoka Hapo Kileleni hadi Mwanza na Dar es salaam.
Angalia pale juu kileleni ndio kuna hayo maandishi hapa chini



Huu ni umbali Kutoka Kileleni mwa mnara wa Eiffel Kuelekea Mwanza.



Na huu ni umbali Kuelekea Dar es salaam.